Ibraah - Nani

Asubuhi kumekucha
Wingu limetanda
Na mvua yata kunyesha
Na uko mbali mama

Maji takitiririka
Oh baridi itanishika
We ndo chanda chema
Uhakika unanikatisha tamaa

Utaambiwa binadamu
Ah kila mmoja ana mapungufu yake
Sijui nilipoteleza mama

Si ungeniambia
Nimemiss tabasamu
Kutwa kucha
Picha kummezea mate

Yangu fimbo umeibeza
Ah katu hautaki kuitumia

Labda hesabu za kutoa
Mi niligawanya baby unisamehe
Na ile hasi nikafanya chanya
Baby unisamehe

Na hata emoji za kulia
Nazo kutumia nazo zikome
Japo nipate furaha
Ah huruma unionee

Maana hii hali, hata haifichiki
Kutwa wima cha mpingo, kisiki
Maana hata nikiona michezo ya njiwa
Ah huwa naitamani
Kama si wewe

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani…

Eh penzi usifanye kwa chombo cha usafiri
Ikawa umeshuka uje utanikatili
Nitakuwaga mental Niko dhahari
Si unasikia

Penzi la dhati daima la wawili
We fanya na urudi lisiwe batili
Ka wafanya kusudi ni ukatili
Mi naumia

We ndo yangu hifadhi
Labda nilikosea msimbo
Kweli kupenda kazi
Wangu umegeuka fimbo o

Mi ndo lako koroboi
Lile lisilo zima
Aha si ulisemaga hauchomoi
Kumbe imani ulinipima ah

Pia ulisema haudonoi
Wameiteka mazima
Ahaa simung'unyi sikohoi
Sina vyangu nimechina

Maana hii hali, hata haifichiki
Kutwa wima cha mpingo, kisiki
Maana hata nikiona michezo ya njiwa
Ah huwa naitamani
Kama si wewe

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda

Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda aah

Written by:

Publisher:
Lyrics © Sentric Music

Lyrics powered by Lyric Find

Ibraah

Ibraah

View Profile